Tuesday, August 2, 2016

Wiki ya Unyonyeshaji Duniani

Nchi zaidi ya nchi 170 duniani zinasherehekea wiki ya unyonyeshaji kuanzia Agosti Mosi hadi Agost 7, ili kuchagiza jukumu la onyonyeshaji kwa lengo la kuboresha afya wa watoto kote duniani.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO kunyonyesha ni njia bora ya kuwapatia watoto wachanga virutubisho muhimu na vya kipekee wanavyohitaji mwilini.

Shirika hilo linapendekeza watoto kupewa maziwa ya mama mara tu anapozaliwa kuanzia saa moja baada ya mtoto kuzaliwa hadi miezi sita.

(Picha kwa hisani ya peacefulearthgracefulbirth.worldpress. com). 
Maziwa ya mama ndio chakula pekee cha mtoto wa kuanzia mwezi sifuri hadi sita kinachomjenga mtoto kimwili, kiakili na kijamii.  
Kunyonyesha sio tendo tu la kumpa mtoto chakula chake bali ni  moja Wapo ya sehemu ya Malezi ya mwanzo. 
Kila  mama anayenyonyesha hufanya mahusiano ya kijamii na mwanae. Mtoto anaponyonya anajifunza upendo kutoka kwa mama ndio maana akinyonya huwa haachi kumwangalia mama yake usoni ili aisome ishara. kadiri anavyoendelea kunyonya mtoto huanza pia kutaka kujaribu mamlaka ya mama kwake. Na hapa mama anapaswa kujua hilo jaribio likichekewa mtoto anakudharau. Ukiwa unamnyonyesha mtoto akakuuma ujue huo sio mchezo. Mkemee haraka sana.Na hatarudia. Kuna maelezo mengi kuhusu hiyo tabia lakini usimng'ate na wewe au kumchapa kibao au chocolate cha kuumiza mwili bali akikuuma mnyime kunyonya kwa wakati huo kisha mpe  aendelee akirudia tena mnyime hadi aelewe titi ni la kunyonya tu sio kuuma. 
Ukifanya hivyo utakuwa umeweka msingi wa kwanza wa kutii mamlaka. 

Hata hivyo kwa Mujibu wa Utafiti uliofanywa na wizara ya afya nchini imebainika kuwa ni asilimia 51% tu ya watoto wenye umri wa Miezi 0 hadi sita  wanaonyenyeshwa kikamilifu. 
Inashauriwa
 Mtoto anyonye hadi umri wa miaka mwili. 
#chochea tabianjema@mnyonyeshemtoto kwa maendeleo
tukutane kesho. 

No comments:
Andika comments

Shukrani

Aina za Habari

Hifadhi