Wednesday, May 25, 2016

Kilimo cha Vitunguu Maji

 Vitunguu ni mojawapo kati ya mazao ya muda mfupi yanayolimwa  kibiashara hapa nchini. Zao hili linawapatia wakulima kipato cha haraka ambacho kinawasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kimaisha na kujikwamua kutoka katika umasikini.
NI WAPI VITUNGUU HUSITAWI?
Hapa Tanzania vitunguu  husitawi katika maeneo ya mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mara,Manyara, Tanga,  Singida na Mbeya. 

Vitunguu husitawi vizuri katika Maeneo yenye mwinuko wa mita 800 -1500 kutoka usawa wa bahari. Hali ya baridi kidogo inafaa sana kwa kitunguu hususan kipindi cha kuotesha mbegu.  Hata hivyo inashauriwa baridi isizidi nyuzi joto 20 hadi 27C. 
 
Inashauriwa mbegu zipandwe kipindi cha baridi ili kivunwe kipindi cha joto. 

UDONGO UPI HASWAA UNAOFAA? 
Kitunguu uhitaji udongo tifutifu wenye rutuba usiotuamisha maji kwa muda mrefu. 
UOTESHAJI WA MBEGU 
Uoteshaji wa mbegu za vitunguu huoteshwa kwanza kwenye vitalu. Vitalu viandaliwe wiki mbili kabla ya kupanda. Mbegu ikishaota itakaa kwenye kitalu kwa muda wa siku 30-40 kabla ya kuhamishiwa shambani. 
Mbegu ya kitunguu ikiwa katika kitalu.
Itaendelea... 


 


No comments:
Andika comments

Shukrani

Aina za Habari

Hifadhi