Monday, August 8, 2016

Ubora wa Maziwa ni kwa kula mlo Kamili .

Kwa mama unayenyonyesha tambua kuwa maziwa anayopata mtoto kutoka  kwako ubora wake hutokana na kile chakula ulichokula ukiwa mjamzito na hadi sasa unaponyonyesha.
Inashauriwa kwa mama anayonyesha kula mlo kamili ili mtoto apate virutubisho vyote muhimu vitakavyojenga afya ya mwili na ya akili na ukuaji kwa ujumla.  

Baadhi ya akina mama huwa wanashindwa kutofautisha kati ya vichocheo vya kuongeza maziwa na ubora wa maziwa. Mfano mama anayejifungua kwa mara ya kwanza huweza kujikuta hatoki maziwa. Kwa kawaida watu walio karibu naye humshauri anywe uji wa pilipili na supu kwa wingi, nyanya chungu,kutafuna mihogo na vingine vingi. Wakati mwingine anaambiwa anywe chai ya tangawizi. Lakini ikumbukwe kuwa huu  sio mlo wa mama anayenyonyesha. Bali ni vichocheo vya kuchagiza maziwa yatoke. Kimsingi kutotoka kwa maziwa kunasababishwa na mmabo mengi ikiwemo kutokuwa tayari kwa mzazi kisaikolojia. kutokuwa tayari kunahusisha hofu au uoga wakati mwingine hekaheka za kipindi cha ujauziti zilimchosha mama, lakini kubwa kuliko yote ni mlo gani alikuwa anakula mama huyo kipindi akiwa mjamzito?
Ubora wa viini lishe vinapatikana katika chakula ambacho kimezingatia Makundi yote  ya chakula.Supu ya mboga mboga ni muhimu sana  kwa ajili ya vitamini. 
Mlo  uliokamilisha makundi yote ya chakula. 

(Picha hii ni kwa hisani ya #wives_and_mothers)
Mama anayekula vizuri maziwa huwa mengi na yenye Ubora. 

No comments:
Andika comments

Shukrani

Aina za Habari

Hifadhi