Sunday, August 14, 2016

Vijimambo vya Ujauzito


Mambo Haya huwezi kuelezwa na daktari

Kipindi cha ujauzito kimejaa mambo mengi ya kustaajabisha. Lakini kwa akina mama watarajiwa kwa mara ya kwanza hujumuisha mambo ambayo hakuyatajaria kuwa ni ya kawaida katika kipindi hicho. Mambo haya pia si rahisi kuambiwa na daktari yeyote. Ila ni muhimu uyajue.

Kuwashwa tumboni
"Katika mwezi wa saba wa ujauzito wangu, nilipatwa na muwasho tumboni kiasi kwamba nilikuwa siwezi kuvumilia” anakumbuka Skola John

Wataalam wa afya ya uzazi na magonjwa ya akina mama wanasema kuwa hali hii inasababishwa na ukavu wa ngozi na kutanuka kwa ngozi kutokana na kukua kwa mtoto. Hivyo inashauriwa endapo utakutwa na hali hii usijikune sana kwani inaweza kusababisha upate alama za mikwaruzo  badala yake jitahidi kujipaka mafuta ya kuainisha ngozi mara kwa mara. Pendelea kupaka Mafuta ya nazi au olive oil.



Hata hivyo kipindi cha ujauzito akina mama wengi pia husumbuliwa na matatizo mbalimbali ya ngozi.Ni muhimu kuwa mwangalifu pindi uonapo dalili ambazo sio nzuri katika ngozi yako ukamuona daktari ambaye ni mtaalam wa mausala yanayohusu ngozi au uendepo kliniki muulize daktari wako akupe mwongozo mzuri wa uhakika.

1 comment:
Andika comments

Shukrani

Aina za Habari

Hifadhi